Lissu: Swali langu la pili umesema kwamba katika moja wapo ya shughuli ulizoshiriki ni pamoja na kungamano la vijana ambalo kwa ushahidi wako halikufanyika sababu uwanjani kulitawanywa
Lissu: Waeleze majaji kama kuna sehemu imeandikwa “uwanjani kulitawanywa”
Shahidi: Hapa ni upungufu tu wa baadhi ya maneno
Lissu: Sio upungufu yapo au hayapo
Lissu: Umesema kwamba hilo kongamano kwa bahati mbaya au nzuri halikufanyika ni kweli sio kweli?
Lissu: Mfuasi wa CHADEMA kongamano lisipofanyika ni bahati nzuri? Kweli si kweli
Shahidi: Ndiyo maana nimesema bahati mbaya au nzuri sijasema nzuri moja kwa moja
Lissu: Ndiyo maana nimekuuliza kama wewe ni pandikizi la polisi
Shahdi: Kama kuna maswali mengine tuendelee hilo nimeshajibu
Lissu: Kwenye ushahidi wako umesema “siku hiyo ukiwa na simu yako” ni kweli sio kweli Shahidi: kweli
Lissu: Waeleze majaji kama maneno “nilikuwa na simu yangu “yapo kwenye karatasi?
Lissu: Unaweza au huwezi kufuatilia mtandao wa Youtube kwa kutumia tarakilishi
Shahidi: Mimi binafsi nimezoea kwenye simu sio tarakilishi
Lissu: Inawezekana haiwezekani
Lissu: Waeleze majaji kama unajua kufuatilia youtube kupitia Television
Lissu: Nirudie swali langu kwenye maelezo yako kuna sehemu umeandika ulikuwa na simu siku hiyo?
Lissu: Umesema siku hiyo uliona video fupi ikimuonesha Mhe. Lissu akihamasisha kuzuia uchaguzi?
Lissu: Kuna mashahidi wamekuja kwenye mahakama hii wamesema hiyo video ina masaa matatu na madakika mengi tueleze kwenye karatasi yako kuna sehemu umeeleza juu ya urefu wa video hiyo
Lissu: Kwenye ushahidi wako umesema unafahamu Tundu Lissu kupiitia mitandao ya kijamii Shahidi: Kweli
Lissu: Kwenye maelezo yako kuna maneno hayo?
Lissu: Kwenye maelezo yako umesema kuwa ukishiriki mkutano uliongozwa na mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu uliofanyika Luanda Nzovwe?
Lissu: Kwa hiyo umewahi kumuona Lissu kwenye mkutano?
Lissu: Umesema kwenye maelezo yako kuwa baada ya kuangalia video hiyo alikufuata akakuita pembeni “njoo tuonge”?
Lissu: Kwenye maelezo yako kuna maneno “njoo tuonge”?
Shahidi anamsomea Lissu maelezo yake
Lissu: Kuna maneno “aliniita pembeni njoo tuongee” yapo au hayapo?
Lissu: Ukasema “niliposogea pembeni akajitambulisha kama askari polisi akaniambia twende kituoni” kweli sio kweli?
Lissu: Waeleze majaji kama maneno hayo yapo
Lissu: Badala yake kuna maneno yanasema hivi “Wakati tunaendelea kubishana kuna mtu aliyejitambulisha kama afisa polisi na akanikamata kwa kuhamasisha vurugu za kuzuia uchgauzi” kwa maelezo yako alikuja na kukumata?
Lissu: Kwa maelezo yako unasema ulipofika polisi alikuweka maabusu na baadaye akakupeleka kwenye chumba cha mahojiano akaniambia “kwa nini unahamasisha uasi” kweli sio kweli?
Lissu: Namsomea shahidi maana ya neno uasi kwenye kamusi kuu ya kiswahili iliyotolewa na BAKITA Uasi- Kitendo cha kuwapinga wenye mamlaka iliyopo kama vile kwenye taasisi, ofisi au chama Mtu akisema atafanya uasi ni kufanya maandamano bila kufuata taratibu waeleze majaji kama kitendo hicho cha kuvunja sheria kama ni uhaini
Lissu: Waeleze majaji kama kupinga mamlaka na sheria za nchi zilizopo ni uhaini?
Lissu: Hapa nina sheria ya uchgauzi ya 2024 na kwenye sheria hiyo hakuna kosa la kuzuia uchaguzi achilia uhaini
Lissu: Sasa naelekea kumalizana na wewe swali langu la kwanza ulipokamatwa tarehe 4-4-2025 ulipelekwa kituoni ukaandika maelezo kwa tuhuma za kupanga kufanya vurugu kuzuia uchaguzi waeleze majaji hizo tuhuma ziliishia wapi?
Shahidi: Niliripoti mpaka nilipoambiwa nitapigiwa simu kuja kutoa ushahidi kuhusu kosa langu Lissu: Umeshtakiwa kwa kosa la kula njama ya kupiga watu mawe kwenye uchgauzi?
Lissu: Ulipanga njama na polisi ili ujifanye mwanachadema uje utoe ushahidi hapa kweli sio kweli?
Lissu: Kwa nini hujapelekwa mahakamani
Lissu: Uliripoti kwa miezi mitano polisi, je polisi wanakuambia nini?
Lissu: Waeleze majaji kama katika kipindi cha miezi mitano kama umewahi kuzungumzia tuhuma zako kula njama na kupiga watu mawe
Lissu: Kwanzia mwezi wa 5 hujawahi kuwasiliana na polisi na mpaka sasa?
Lissu: Ulifikaje Dar es salaam
Shahidi: Nilipigiwa simu na mtu aliyejitambulisha ni askari nikapewa wito wa kuja mahakamani Lissu: Nauli alikulipia nani?
Shahidi: Nimejilipia mwenywe
Lissu: Hapa Dar umefikia wapi?
Lissu: Sitaki kujua ni gesti gani ila nani analipia?
Lissu: Kwa hiyo umekuja kwa kujitolea kama raia mwema? Lissu amemaliza kuhoji