Madaktari wa sudan wasema raia 28 wameuawa katika shambulio la RSF kaskazini Darfur
Na Alfred Lasteck
Takriban raia 28 wameuawa na wengine 39 kujeruhiwa kufuatia shambulio katika eneo la Mustariha, jimbo la Kaskazini Darfur nchini Sudan.
Kwenye taarifa iliyotolewa Jumanne, Mtandao wa Madaktari wa Sudan (Sudan Doctors Network) ulisema eneo hilo lishambuliwa na wanamgambo wa RSF, vikiangamiza kituo pekee cha afya kilichokuwepo eneo hilo.
Idadi ya waliopoteza maisha na kujeruhiwa inachukuliwa kuwa ya awali.
“Wafanyakazi wa afya waliokuwa wakienda kazini pale walishambuliwa, na mfanyakazi mmoja wa afya alikamatwa na hadi sasa hajapatikana,” ilisema taarifa hiyo.
Madaktari wa Sudan wamekosoa kitendo hicho, wakiitaka RSF kusitisha hofu kwa wakazi na kuzingatia makini mahitaji ya huduma za afya, huku wakidai kuwa mashambulio hayo yalikusudia kuathiri vituo vya afya.
RSF bado haijatoa kauli yoyote kuhusu madai hayo.
Mtandao wa madaktari ulisema vurugu hizo zimesababisha makundi ya watu kuhamia vijiji jirani na kuongezea hali mbaya za kibinadamu zilizokuwepo tayari katika eneo hilo.
Kaskazini Darfur imekuwa ikishuhudia mapigano makali katika miezi ya hivi karibuni, huku migongano kati ya jeshi la Sudan na RSF ikiendelea kuharibu sehemu za nchi.
Kulingana na Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO), mashambulio matano dhidi ya vituo vya afya nchini Sudan yameripotiwa mwaka huu, yakiua watu 69 na kujeruhi wengine 49.
Wakati huo huo, Madaktari wasiokuwa na mipaka, Médecins Sans Frontières (MSF) wanasema walitibu wagonjwa karibu 170 waliopata majeraha yanayohusiana na mashambulio ya drone katika wiki mbili za mwanzo za Februari.
Pia Unaweza kusoma: