Moja kwa moja, Ujumbe wa Iran upo Pakistan kwa mazungumzo

Hata hivyo, msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Iran amesema hakuna mipango ya mazungumzo ya ana kwa ana kati ya pande hizo mbili, akibainisha kuwa ujumbe wa Iran utawasilishwa kupitia Pakistan.

Moja kwa moja

Na Yusuph Mazimu

  1. Araghchi hayupo Pakistan kuzungumzia nyuklia - Iran

    d

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, hana “jukumu lolote linalohusiana na mazungumzo ya nyuklia” katika ziara yake nchini Pakistan, kwa mujibu wa mkuu wa kamati ya usalama wa taifa ya Iran.

    Akizungumza na waandishi wa habari mjini Tehran jana usiku, Ebrahim Azizi alisema waziri huyo yuko Islamabad “kwa ajili ya mazungumzo ya mahusiano ya pande mbili pekee.”

    Azizi ambaye pia ni kamanda wa zamani wa Jeshi la walinzi wa mapinduzi ya kiislamu (IRGC) alisema masuala ya shughuli za nyuklia “yanabaki kuwa moja ya mipaka mikuu ambayo Iran haiwezi kuvuka.”

    Kwa upande mwingine, Marekani imeitaka Iran kusitisha mpango wake wa nyuklia, ikisisitiza kuwa hilo linapaswa kuwa sehemu ya makubaliano yoyote ya mwisho ya amani.

  2. Marekani yazuia meli nyingine ya Iran

    a

    Chanzo cha picha, CENTCOM

    Jeshi la Marekani limesema limefanikiwa kuiizuia meli nyingine iliyokuwa na bendera ya Iran ikiwa njiani kuelekea bandari ya Iran, kama sehemu ya hatua za kuimarisha mzingiro wa baharini dhidi ya nchi hiyo.

    Kwa mujibu wa taarifa kutoka jeshi la nchi hiyo, operesheni hiyo ilifanyika Aprili 24, ikiongozwa na manowari ya kivita ya USS Rafael Peralta, ambayo ilitekeleza hatua za kudhibiti usafiri wa majini unaohusishwa na Iran.

    Hatua hiyo ni sehemu ya juhudi pana za Marekani za kuzuia biashara ya mafuta ya Iran na kukata vyanzo vya mapato ya nchi hiyo, hasa kufuatia mvutano unaoendelea kati ya pande hizo mbili.

    Mvutano huo umeongezeka katika wiki za karibuni baada ya Marekani kufanya mashambulizi ya kijeshi na Iran kujibu kwa kuzuia baadhi ya njia muhimu za usafirishaji wa mafuta katika eneo la mlango bahari wa Hormuz, jambo lililoathiri usafirishaji wa nishati duniani na kuongeza bei ya mafuta.

  3. Marekani yaongeza shinikizo la kiuchumi dhidi ya Iran

    Marco Rubio, US secretary of state

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Marco Rubio

    Marekani imetangaza kuongeza shinikizo la kiuchumi dhidi ya Iran, ikisema inachukua hatua “madhubuti” kuvuruga biashara haramu ya mafuta ya nchi hiyo.

    Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imesema hatua hizo zinajumuisha vikwazo vilivyowekwa na Marekani dhidi ya kiwanda kikubwa cha kusafisha mafuta nchini China pamoja na maeneo mengine 40.

    Kwa mujibu wa Marekani, taasisi hizo ni “mishipa muhimu ya kifedha” kwa utawala wa Iran, zikichangia kufadhili shughuli zinazoelezwa kuwa za “kuleta machafuko” katika eneo la Mashariki ya Kati.

    Taarifa hiyo imeongeza kuwa vikwazo hivyo vinalenga kukata mtiririko wa fedha unaosaidia biashara hiyo ya nishati, huku Marekani ikiahidi kuimarisha zaidi kampeni yake ya shinikizo la kiuchumi dhidi ya Iran na mtandao wa kimataifa unaoiunga mkono.

  4. Iran yafika Pakistan kwa mazungumzo, Marekani yasubiri mapendekezo ya Tehran

    s

    Chanzo cha picha, Reuters

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi, amewasili Islamabad, Pakistan kwa mazungumzo yanayolenga kufufua juhudi za amani kati ya Iran na Marekani baada ya wiki nane za mvutano mkubwa wa kijeshi.

    Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema Iran inatarajiwa kuwasilisha mapendekezo yanayoweza kukidhi matakwa ya Washington, ingawa hakufafanua maelezo ya mapendekezo hayo.

    Hata hivyo, msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Iran amesema hakuna mipango ya mazungumzo ya moja kwa moja kati ya pande hizo mbili, akibainisha kuwa ujumbe wa Iran utawasilishwa kupitia Pakistan.

    Wakati huo huo, wajumbe maalum wa Marekani, Steve Witkoff na Jared Kushner, wanatarajiwa kuwasili Pakistan kwa mazungumzo hayo, huku Ikulu ya White House ikisema Washington iko tayari kutoa nafasi kwa diplomasia.

    Mvutano kati ya Iran na Marekani umeendelea kuathiri masoko ya dunia, hasa baada ya Marekani kufanya mashambulizi ya anga na Iran kuzuia njia muhimu ya usafirishaji mafuta ya Strait of Hormuz, hatua iliyochangia kupanda kwa bei ya mafuta duniani.

    Pande zote mbili zinaonekana kutafuta njia ya kusitisha mgogoro huo, ingawa bado kuna kauli zinazokinzana kuhusu uwezekano wa kufikiwa kwa makubaliano.

  5. Habari na karibu katika habari zetu za moja kwa moja

Trending Now