Makamu wa Rais Iran amtolea maneno makali Trump kufuatia shambulizi la chuo kikuu Tehran

Chanzo cha picha, Getty Images
Makamu wa kwanza wa rais wa Iran ameita shambulizi katika Chuo Kikuu cha Teknolojia cha Sharif "ishara ya wazimu na ujinga wa Trump". Hata hivyo, Marekani bado haijathibitisha kuwajibika katika shambulizi hilo.
Inaonekana shambulizi hilo limeharibu sehemu za chuo kikuu, ikiwa ni pamoja na jengo lake la kituo cha teknolojia na msikiti wa shule hiyo, BBC Persian inaripoti. Shambulizi hilo pia limesababisha kukatika kwa gesi katika sehemu za Tehran.
Dkt. Mohammad Reza Aref amesema rais wa Marekani "anashindwa kuelewa kwamba maarifa ya Iran hayajawekwa kwenye majengo ili yaharibiwe na mabomu; ngome ya kweli ni mapenzi ya maprofesa na wasomi wetu".
"Ngome hii haitaporomoka," ameongeza.
Vyuo vikuu kadhaa nchini Iran vimeathiriwa tangu kuanza kwa vita, vikiwemo Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Tehran na Chuo Kikuu cha Shahid Beheshti.
Soma zaidi:







