Tundu Lissu arejea tena Mahakamani Tanzania
Kesi ya uhaini dhidi ya Kiongozi wa Upinzani nchini Tanzania inaendelea kusikilizwa jijini Dar es Salamaa.
Muhtasari
- Kimbunga chauwa watu 59 Madagascar
- Mshukiwa wa mauaji ya Bondi Beach afikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza
- Kesi ya Tundu Lissu yaahirishwa hadi kesho
- Tundu Lissu aanza kumuhoji Shahidi P8
- Mgomo wa usafiri wa anga wavuruga safari za ndege Kenya
- Lissu Mahakamani: Kesi yaahirishwa hadi Jumatatu
- AU yapinga kuundwa kwa serikali mbadala Sudan
- Tarique Rahman kutangazwa Waziri Mkuu mpya wa Bangladesh
- Rubio: Tunaishi katika 'enzi mpya' ya siasa za kijiografia
- Tundu Lissu: 'Mheshimiwa nataka kuonesha kuwa shahidi ni muongo na hapaswi kuaminika'
- Shahidi: 'Nilikuwa nimevalia T-shirt yangu ya 'No Reform No Election'
- Kesi ya Lissu: 'Nilipata taarifa kwamba Mwenyekiti amekamatwa Wilaya ya Mbinga
- Kesi ya Tundu Lissu: Shahidi P6 aendelea na ushahidi
- Kesi ya Tundu Lissu: Yaliojiri hapo Jana kwa ufupi
- Mpaka wa Kenya na Somalia unatarajiwa kufunguliwa tena baada ya takriban miaka 15
- Mmiliki mwenza wa Man United Sir Jim Ratcliffe aomba msamaha kwa matamshi yake
- Thomas Partey akabiliwa na mashtaka mawili zaidi ya ubakaji
- Japan inasema imeikamata meli ya China huku kukiwa na mvutano na Beijing
- Iran yaimarisha kambi ya chini ya ardhi karibu na eneo la nyuklia, picha za satelaiti zaonyesha
- Wanajeshi wa Marekani waondoka katika kambi ya kijeshi ya Tanf nchini Syria
- Trump: Itakuwa "chungu sana" kwa Iran ikiwa hakuna makubaliano
Moja kwa moja
Na Abdalla Seif Dzungu, Beldeen Waliaula na Ambia Hirsi
Afrika Kusini kutumia wanajeshi kukabiliana na magenge ya wahalifu

Chanzo cha picha, Getty Images
Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa, amesema atatuma wanajeshi kuwasaidia polisi kupambana na magenge yaliyojihami na uchimbaji haramu wa madini nchini humo.
Magenge yaliyojihami yamekuwa tishio kubwa katika usalama wa Afrika kusini, taifa ambalo limerekodi idadi ya juu ya visa vya mauaji. "Magenge yaliyojihami kwa sasa wanatishia demokrasia yetu, jamii yetu na ukuaji wa Uchumi," Ramaphosa alisema katika hotuba yake kwa taifa siku ya Alhamisi.
"Nitatuma jeshi la Afrika Kusini (SANDF) kuwasaidia polisi," aliongezea Ramaphosa.
Mwezi uliopita, Waziri wa Usalama wa Ndani Firoz Cachalia, alisema polisi bado hawajafanikia kukabiliana na magenge yaliyojihami.
Ramaphosa pia amewataka machifu, polisi na jeshi kubuni utaratibu utakaotoa mwongozo wa ni wapi vikosi vya usalama vinafaa kutumwa katika siku zijazo.
Aliongezea kuwa wanajeshi hao wataanza na Wilaya ya Western Cape na Gauteng, ambayo yanapakana na miji ya Cape Town na Johannesburg.
"Watoto katika eneo la Western Cape hujipata katikati ya makabiliano makali ya magenge hayo.
Watu wanafukuzwa majumbani kwao na wachimbaji haramu wa madini eneo la Gauteng" Alisema Ramaphosa
Rais huyo wa Afrika Kusini pia alitangaza kuwaajiri maafisa 5,500 zaidi wa polisi, ili kupambana na uhalifu uliokithiri pamoja na kuimarisha idara ya ujasusi.
Habari za hivi punde, Lissu Mahakamani: Kesi yaahirishwa hadi Jumatatu

Kesi ya Kiongozi wa Upinzani nchini Tanzania Tundu Lissu imeahirishwa hadi Jumatatu asubuhi saa tatu.
Kesi hiyo imekuwa ikiendelea katika Mahakama Kuu ya Dar es Salaam kwa siku kadhaa wiki hii.
Mashahidi wa upande wa Serikali leo wametoa ushahidi wao huku Mshatakiwa akipata furas ya kuwahoji.
Shukrani kwa kutufuatilia kwenye Tovuti na mitandao yetu ya kijamii tangu tulipianza kukuljuza yote yanayojiri.
Ungana nasi Jumatatu asubuhi kwa taarifa za moja kwa moja kuhusu kesi ya Lissu kutoka Mahakamani.
Habari za hivi punde, Wakili wa serikali sasa anauliza maswali ya dodoso kwa shahidi.
Wakili wa serikali: Ieleze mahakama kwanini maeleze uliyotoa mahakamani na kwenye ushahidi wako ni tofauti ilhali ulimweleza mshitakiwa hakuna utofauti?
Shahidi: Hayana utofauti bali hapa mahamani nimetoa ufafanuzi na maelezo ya ziada kulingana na maswali ya Jamuhuri
Wakili wa serikali: Swali la mwisho mshitakiwa alipokua akikuuliza swali la mwisho alikuuliza anashitakiwa na kosa gani ulisema haujui hebu iambie mahakama
Shahidi: Mheshimiwa ninaelewa anakabikiwa na kesi ya uhaini kutokana na kauli aliyoitoa ya kutaka kuzuai uchaguzi
Jaji: Shahidi tunakushukuru Mahakama inakushukuru umemaliza kutoa ushahidi wako.
'Nataka ujibu kiaskari': Lissu aendelea kumhoji shahidi wa serikali

Lissu: Swali langu la pili umesema ulijiunga na jeshi mwaka 2012 na ukafuzu mwaka 2013 waleze majaji kama yapo shahidi Sikuyaandika hayo
Lissu: Sema kwa sauti kaka
Shahidi: Nimesema kwa sauti sikuyaandika hayo
Lissu: Kwa ushahdi wako umesema ulipata mafunzo kwenye shule ya upolisi iliyoko Moshi
Shahidi: Hakuna
Lissu: Nataka ujibu kiasakari ...Sasa shahidi twende kwenye yaliyotokea tarehe 8 april 2025 umesema baada ya kumkamata huyu kijana umesema RCO alikuelekeza ufungue faili la uchunguzi. Nataka kujua RCO alisema muandike maelezo na awekwe mahabusu mpaka mtakapopata maelekezo mengine?
Shahidi: Waheshimiwa maelezo hayo yapo ila nimeifafanulia mahakama ila hilo la akae mahabusu mpaka maelekezo mengine sikuliandika
Lissu: Umeeleza kwamba huyu mtuhumiwa aliwekwa rumande na baadae akaachiwa kwa masharti ya kuripoti kila jumatatu?
Shahidi: kwenye maelezo yangu hakuna
Lissu: Asante kwenye maelezo yako hakuna, sasa shahidi nikulete kwenye kilichotokea RCO alipokuelekeza umtafute huyo kijana tarehe 22 na umuandikishe maelezo upya ya shahidi
Shahidi: Waheshimiwa hilo lipo ila kuna mengine hayapo
Lissu: Kipi kilichohamasisha vijana wenzake kufanya vurugu yapo hayapo?
Lissu: Haya maneno alisema alikuwa anaunga mkono kauli ya mwenyekiti wake wa chama Tundu Lissu
Shahidi: Mheshimiwa Jaji haya mengine sikuyaeleza hapa
Lissu: Na umesema kwamba huyu kijana alikuambia kwamba wamedhamiria kufanya uasi dhidi ya serikali ya CCM
Shahidi: Mheshimiwa kwenye hii aya hakuna
Lissu: Pia umesema kwamba huyu kijana alikuambia kuwa watakinukisha hayo maelezo yapo?
Shahdi: Hayapo yako huku mwanzo
Lissu: unasema kwamba huyu P8 alikuambia kwamba watakinukisha mpaka serikali itakapofanya mabadiliko ya uchaguzi na katiba mpya yapo hayapo
Shahidi: Hayapo
Lissu: Sasa shahidi naomba uwaeleze majaji kama umeeleza sababu ya maelezo yako polisi na ushahidi wako kutofautiana kiasi hiki
Shahidi: Mheshimiwa sijaeleza sababu, sababu hakuna utofauti
Lissu: Ahsante bwana Koplo Lissu: umeeleza kwamba ulimkamata huyu PA ndipo RCO akakuambia fungua faili
Shahidi: tulimkamata baada ya kupata taarifa ndipo tukafungua faili
Lissu: Naam ndio ninachouliza mnakamata ndipo mnaenda kuchunguza na kumpa kesi
Lissu: Mtu anayepanga kufanya Vurugu anafanya kosa la Jinai kweli si kweli
Shahidi: kweli
Tundu Lissu Mahakamani: Shahidi ahojiwa na mshtakiwa

Mshatakiwa ameanza kuwauliza maswali shahidi wa upande wa serikali Koplo Michael.
Jaji amemuuliza mshitakiwa kama ana maswali ya Dodoso.
Lissu akamjibu mengi na kuendelea kusema; Nyie wenye watoto mkipeleka watoto polisi wanaenda kupata dhambi za uongo.
Lissu: Shahidi detective Michael naomba nikuhoji kama uliandika maelezo yako ya ushahidi.
Lissu: Naomba Uwaeleze Majaji iwapo utayatambua
Shahidi: Ndio nitayatambua
Lissu: Mheshimiwa Jaji naomba shahdi apewe maelezo yake.
Shahidi: Nimeyaoana maelezo haya ya tarehe 24/4/2025 na nimeyatambua yana sahihi yangu
Lissu: Waheshimiwa naomba nimuulize maswali machache kufahamu ukweli wa shahidi huyu ...Lissu ana msomea shahdi maelezo yake yote Kisha anamuomba shahidi kama melezo yake yapolewe kama kielelezo
Shahidi anasema kwa kuwa maelezo ni yake na upande wa Jamuhuri utarudhia basi yuko tayari yapokelewe na upande wa mashitaka
Wakili wa serikali: Ni sawa hakuna pingamizi
Jaji; Maelezo hayo yamepokelewa na yatatambulika kama kielelezo D5
Lissu: Asante waheshimiwa, naomba shahdi apewe kilelezo D5 Umeileza mahakama kwamba wewe ni askari polisi ofisi ya RCO Kilimanjaro tangu 2015 naomba waeleze majaji kuwa hayo maneno kama yapo
Shahidi: yapo ila mwaka ndio hakuna.
Lissu Mahakamani: Mashahidi wa serikali watoa ushahidi
Kesi ya uhaini dhidi ya kiongozi wa upinzani nchini Tanzania Tundu Lissu inaendelea katika Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam baada ya kuahirisha hapo awali.
Shahidi wa upande wa serikali Koplo Michael, Mkuu wa Upelelezi MkoaNI Kilimanjaro amekula kiapo na kuielezea Mahakama kilichotokea mwezi wa nne 2025.
Wakili wa Serikali - Tarehe mwezi wa nne 2025 unakumbuka nini
Shahidi: nilikuwa doria na askari wenzangu ambapo tulikuwa tunazunguka maeneo mbali mbali ya Moshi mjini yani wilaya ya Moshi Mjini.
Wakili wa serikali: Mlikuwa na lengo gani
Shahidi: Lengo ilikuwa kudhibiti uhalifu na kuwalinda raia na mali zao - [ ] Nakumbuka siku hiyo nilipofika maeneo ya Njoro iliyopo Moshi tulipata taarifa za kiintelijensia kuwa kuna kijana mmoja anahamasisha wenzake kuhusiana na kufanya vurugu katika uchaguzi mkuu ujao uliokua unakaribia kufanyika mwaka 2025
Wakili wa serikali: Bada ya kupata hizo taarifa mlichukua hatua gani
Shahidi: Baada ya kuoata hizo taarifa tuliende eneo la alipokuepo huyo kijana kama tulivyopewa taarifa na kumkamata huyo kijana
Wakali: Nini kilifuata
Shahidi: Tulimpeleka mpaka ofisi ya RCO Mkoa wa Kilimanjaro
Wakili: Nini kilifuata
Shahidi: Tulimfahamisha Mkuu wa Upelelezi ACP Abichi Malanga na kunielekeza nifungue jalada la uchunguzi
Wakili: Na wewe ukafanya vipi
Shahidi: Nilifungua Jalada kesi nambari ar/cid/ee/18/2025
Wakili: Nini kilifuata baada ya kufungua jalada
Shahidi: Afande RCO alisema kijana huyo ahojiwe na alihojiwa na detective Koplo Rashid
Wakili: Nini kikafuata
Shahidi: Pia alitoa maelekezo awekwe mahabusu na kuongeza kuwa atatoa maelekezo ya nini kitakachofuata baadae.
Wakili: Nini kilifuata
Shahidi: Kijana huyu alitolewa kwa masharTi baada ya kukaa mahabusu kuwa angekuwa anakuja kuripoti polisi
Wakili wa serikali: Nini kilifuata
Shahidi: Ilipofuka tarehe 22/04/2025 afande RCO alinipa maelekezo ni mtafute yule kijana ambaye anakuja kuripoti na nimuandikie maelezo upya.
Wakili: Maelezo ya aina gani
Shahidi: Maelezo ya shahdi aeleze ni kitu gani kilichopelekea yeye kuhamasisha vijana wenzake kufanya vurugu katika uchaguzi mkuu uliokuwa unatarajiwa 2025.
Wakili: Wewe ulifanya nini
Shahidi: Nilienda kwenye kumbukumbu na kuchukua mawasiliano yake na bahati nzuri siku hiyo alikuwa amepangiwa kuripoti
Wakili: Nini kiliendelea
Shahidi: Nilitoa maelekezo kwa askari wanaohusika na kuwahudumia hao wanaokuja kuripoti kuwa akifika awasiliane na mimi .Alipofika niliandika maelezo yake kwenye karatasi ya maelezo ya shahidi
Wakili:alikueleza nini kwa ufupi
Shahidi: Alinieleza yeye ni mwanachama wa chama cha Chadema na amelikuwa mwanachama tangu akiwa sekondari
Mashahidi upande wa serikali wamemaliza kutoa ushahdi wao na kinachofuata ni maswali ya upande wa mshatakiwa.
AU yapinga kuundwa kwa serikali mbadala Sudan

Chanzo cha picha, Getty Images
Baraza la usalama na amani la Umoja wa Afrika, limepinga vikali kuundwa kwa '‘serikali mbadala’' nchini Sudan.
Baraza hilo linaonya kuwa hatua hiyo itakandamiza uhuru, umoja na kuheshimu kwa mipaka ya taifa hilo.
Taarifa iliyotolewa na kundi la Sudan Founding Alliance, muungano unaohusishwa na kundi la wapiganaji wa Rapid Support Forces (RSF), ambao walitangaza kuunda serikali mbadala nchini Sudan.
Umoja wa Afrika umetaka mataifa wanachama na jamii ya kimataifa, kutoitambua wala kutoiunga mkono serikali hiyo ya RSF.
Muungano huo ambao unajiita Leadership Council of the Sudan Founding Alliance (TASIS), unaongozwa na kiongozi wa RSF Jenerali Mohamed Hamdan Dagalo, maarufu kama Hemedti.
RSF awali ilikuwa imetangaza mipango yake ya kuunda serikali itakayoiongoza eneo la magharibi mwa Sudan, ikiwemo kuwateua viongozi na mawaziri.
Mwezi Agosti 2025, baraza la usalama la umoja wa mataifa ilipinga tangazo la RSF la kuunda serikali mbadala na kusema hatua hiyo itadhoofisha zaidi mgogoro wa kibinadamu unaoshuhudiwa nchini humo.
Vita wenyewe kwa wenyewe nchini Sudan vilianza mwezi Aprili mwaka wa 2023, baada ya mvutano wa madaraka kati ya kikosi cha RSF na jeshi la Sudan (SAF).
Maelezo zaidi:
Tarique Rahman kutangazwa Waziri Mkuu mpya wa Bangladesh

Chanzo cha picha, NurPhoto via Getty Images
Chama cha Bangladesh Nationalist Party (BNP) kinaongoza katika uchaguzi mkuu uliofanyika nchini humo, huku kiongozi wa chama hicho Tarique Rahman, akitarajiwa kutangazwa kama Waziri Mkuu wa taifa hilo.
Huu ni uchaguzi wa kwanza kufanyika baada ya maandamano makubwa kushuhudiwa nchini humo mwaka wa 2024, na kumuondoa madarakani aliyekuwa Waziri mkuu Sheikh Hasina.
Mpinzani mkuu wa chama cha BNP ni Jamaat-e-Islami ambacho kimetilia shauku matokeo ya uchaguzi huo.
Chama cha BNP kinaongoza kwa kuchukua viti zaidi ya theluthi mbili vya bunge. Kiongozi wa sasa Muhammad Yunus, ambaye anatarajiwa kujiuzulu baada ya serikali mpya kuchukua madaraka amewataka raia wa taifa hilo kudumisha amani.
Soma pia:
Katika taarifa zingine Rubio asema: Tunaishi katika 'enzi mpya' ya siasa za kijiografia

Chanzo cha picha, Reuters
Waziri wa Mambo ya nje wa Marekani Marco Rubio, anasema ni ulimewengu uko katika ''enzi mpya’'
Amesema hayo katika ziara yake ya Ulaya huku akitarajiwa kutoa hotuba katika kongamano la usalama mjini Munich.
Hii ni ziara ya kwanza ya wajumbe wa Marekani kuhudhuria kongamano la kimataifa barani Ulaya, baada ya Rais Trump kutishia kuliichukua eneo la Greenland.
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, amesisitiza kuwa lazima Ulaya ijikomboe kutoka kwa Marekani, huku Katibu Mkuu wa Jumuiya ya kujihami ya Nato, Mark Rutte, akisema uhusiano wa mataifa ya transatlantic bado uko imara.
Vita vya Ukraine, wasiwasi ulioko China, na mazungumzo ya nyuklia kati ya Iran na Marekani inatarajiwa kujadiliwa katika mkutano huo wa Munich "Dunia inabadilika kwa kasi sana," Rubio aliwaambia wanahabari.
Alipoulizwa iwapo ujumbe wake kwa ulaya utakuwa wa utangamano alijibu kuwa; "Tunaishi katika enzi mpya ya siasa za kijiografia, na itatulazimu tutathmini jinsi hali ilivyo na wajibu wetu utakuwa upi".
Katika kongamano la mwaka uliopita, Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance, aliishambulia Ulaya, ikiwemo Uingereza kuhusu sera zao za uhuru wa kujieleza na uhamiaji.
Lissu Mahakamani: Kesi yaahirishwa hadi saa nane
Lissu amaliza kumhoji shahidi
Lissu: Naweza ondoa hili swali, maandamu wanasema wana mlinda shahidi lakini kielezo D4 kina taarifa zote za shahidi mpaka jina, umri makazi na dini licha ya mahakama kueleza shahidi alindwe.
Jaji: Kama umeridhia kuendelea bila kutolea uamuzi ni sawa tuendelee.
Lissu: Shahidi, umesema wewe ni mwanachama wa Chadema kwenye kilele D4 polisi ulisema wewe ni mwanachama wa chadema
Shahidi: Hapana
Lissu: Waeleze majaji tangu ulipoandika maelezo hayo umewahi kwenda polisi kuandika maelezo mengine au kupelekea taarifa nyingine yoyote polisi kuhusiana na kesi hii?
Shahidi; Hapana
Lissu: Waleze maajaji kama umetoa tarifa polisi kama kuna mtu yeyote anakutishia maisha baada ya tarehe 25/04/2025 kama kuna kiongozi au mfuasi wa Chadema aliyekutishia maisha
Shahidi: Hapana
Lissu: Waleze majaji kama kuna mtu yeyote Chadema aliyekutishia sababu ya kutoa maelezo haya polisi.
Shahidi: Hapana
Lissu: Waeleze majaji kama kuna mtu ametishia kuwadhuru ndugu zako baada ya kutoa maelezo haya polisi
Shahidi: Hapana
Lissu: Sina maswali mengine Mheshimiwa.
Upande wa mashitaka unaomba ahirisho la saa moja waandae mashahidi ikiwa ikiwa ni pamoja na maswala mengine ya kibinadamu.
Lissu anaendelea kumuliza shahidi kwa maswali
Lissu: Naomba ni kuulize maswali mengine baada ya kukupitisha maelezo yako ya polisi. Waeleze majaji kama kiongozi wa chama kama mimi kuita mkutano na kusema tutazuia uchaguzi kama hakuna mabadiliko ni kosa la jinai
Shahidi; Sifahamu
Lissu: Waleze Majaji kama kuna sheria inayokataza kusema tutazuia uchaguzi
Shahidi: Sifahamu
Lissu: Waeleze majaji kwamba kutaka kuzuaidi uchaguzi si kosa la jinai
Shahdi: Sifahamu
Lissu: Waeleze majaji kama ni halali au si halili kwa chama kama Chadema kufanya mkutano wa hadhara popote nchini
Shahidi: Hilo sifahamu. Waeleze majaji kama una fahamu
Lissu: Polisi wa Tanzania hawana mamlaka ya kukataza kutoa vibali vya maandamano au mikutano hawana vibali.
Shahdi Sifahamu
Lissu: Waleze majaji kama unafahamu mikutano iliyozuiliwa ilikuwa imetolewa taarifa siku mbili kabla ya mkutano
Shahidi: Sifahamu
Lissu: Wewe si umesema ulihamasika na Chadema wewe?
Shahidi: Hilo mimi sifahamu
Lissu: Kuvaa fulana iliyoandikwa maandishi no reforms no election kwenye matembezi ni kosa sio kosa?
Shahidi embu tuzungumze kidogo juu ya kukamatwa kwako umesema tarehe 20/04/2025 mkiwa eneo mlilopanga kuanzia matembezi mlikamatwa kweli sio kweli:
Shahdi: Kweli
Lissu: Waliwakamata sababu mlikuwa mnapanga kufanya maandamano bila ya kibali Lissu na waliwapeleka polisi na kutoa melezo shahidi kweli
Lissu: Hayo melezo yako wapi
Shahidi: Mimi sifahamu
Lissu: Hizo tuhuma za kupanga maandamano bila kibali hiyo kesi iliishia wapi ulipelekwa mahakamani?
Shahidi: Ndio
Lissu: Kesi namba ngapi
Shahidi Kesi ilikua inasinamiwa na kaka yangu kwa hiyo sifahamu
Lissu: Kwa hiyo ulishitakiwa
Shahidi: Mimi sifahamu sababu kesi alikuwa anasimamiwa kaka yangu
Lissu; Ndugu yako ni wakili
Shahidi: Mimi sifahamu
Lissu: Waeleze majaji ilikuwaje kesi yako ya kupanga njama ikapotea na sasa ni shahidi kwenye kesi ya uhaini ya unayemuita mwenyekiti wako
Shahidi: Mimi sifahamu Lissu sasa shahidi
Shahidi: Ndio
Mheshimiwa Lissu: Wewe ni mwanachama wa Chadema
Shahidi: Ndio
Lissu: Waeleze majaji umejiunga na chama lini -
[ ] Wakili wa serikali huyu ni shahIdi anayelindwa kupata hizo taarifa kutarahisisha kumtambua shahidi
Kimya kidogo
Tundu Lissu anaendelea kuuliza maswali kwa shahidi P6
Lissu: Ulikuwa na bando la internet hayo maneno yapo hayapo
Shahidi: Hayapo
Lissu: shahidi kwenye ushahidi wako uneeleza kwa kutumia simu yako uliingia kwenye mtandao wa jambo TV
Shahidi: hapana nimeeleza niliingia kwenye akaunti ya jambo TV Lissu: ahsante kwemye maelezo yapo hayapo Shahidi: Hayapo
Lissu: kwenye ushahidi wako umeeleza kwamba kwenye hiyo video uliona nikisema kuwa anayetaka kwenda nasi tutaenda naye na asiyetaka tutamuacha
Shahidi: Ndio
Lissu: waeleze majaji kama kwenye maelezo yako ya polisi yapo hayo
Shahidi: hayapo Lissu: umesema nilitoa kauli ifuatayo kama kuna anayetaka kugombea udiwani asahau ubunge asahau na mimi uraisi nimeusahau
Shahidi: Ndio
Lissu: Je kwenye maelezo yako ya polisi Shahidi: yapo nilisema polisi ila hapa hayapo
Lissu: Je, kuna mahali popote umeandika kwenye maelezo ya polisi ulikuwa na simu?
Shahidi: hilo swali ushauliza nikakujibu Lissu: Hapana sijakuuliza Shahidi: ndio kuna mahali nimesema nilikuata na mwenyekiti akaniunga kwenye kundi la watsap hiyo inaonesha nilikuwa na simu
Lissu: Kwenye ushahidi wako umesema nilikuwa nimevaa kombati za kaki waeleze majaji kama kwenye maelezo yako yapo shahidi: sijaona
Lissu: Naomba ni kuulize kidogo kuhusu huyu Esau chiza umemtambulisha kama katibu na kwingine kama mwenye kiti tushike lipi shahidi: 2024 alikuwa katibu 2025 alikuwa mwenyekiti
Lissu: Kwenye maelezo yako 2025 unasema ulimfata katibu je hapo tushike lipi Shahidi: Polisi labda walikosea kuandika Lissu: umesema maneno yangu yalikuhamasisha waeleze majaji kama maneno ya kukinukisha na kufanya vurugu kama yako kwemye maelezo yako polisi
Shahidi: Yapo Lissu: Twende tarehe sita kuwa tarehe sita Lissu atazuru songea na ulipata taarifa toka kwa Esau Chiza waeleze majaji kama yapo kwenye kieleezo polisi
Shahidi: Yapo Nilipata taarifa kuwa mwenyekiti wa chadema taifa…..anasita hapaonekani vizuri
Lissu: leta nikusomee Imeandikwa nilipigiwa simu na Esau Chiza na akanieleza kuwa kuna ziara ya mwenyekiti wilaya ya Songea
Lissu: Je kuna maneno Tundu Lissu?
Shahidi anarudi kusoma na kusema …. kuwa ataongozana na viongozi.
Lissu: shahidi twende siku ya tarehe 10 umesema hivi kwemye ushahidi wako mkiwa na wenzako mkiwa mmekusanyika na wenzako kwenye viwanja vya shule ya msingi makarawe gari ya polisi ikaja na kuwatawanya Je yapo kwenye maelezo yako?
Shahidi: hayo maelezo tulitawanywa hayapo Lissu: Umesema baada ya kutawanywa mlipofika ofisi za chama mfaranyaki polisi walifika na kuwapiga mabomu je hayo maneno mlipigwa mabomu yapo
Shahidi: Tulitawanywa …… Lissu: mlipigwa maboumu kaka Shahidi kimya.. shahidi: mimi ni binadamu siezi kumbuka kila kitu
Lissu: yapo hayao Shahidi: hayapo
Tundu Lissu amkosoa shahidi
Lissu anamaliza kusoma, Hayo ndio maelezo uliyoandika polisi ?
Shahidi: Ndio
Lissu: Kuna maeneo kadhaa nataka kukukanusha eneo la kwanza dini yako la pili umri wako la tatu ni kwenye shughuli za chama uliambiwa utakua unaongoza shughuli za chama kwa bendera?
Eneo la nne ulisema ulipokua kazini ulikuwa na simu ya infinix kwenye maelezo ya polisi haipo
Eneo la tano ni ushahidi wako kuwa ulikuwa na bando kwenye maelezo ya polisi haipo
Eneo la sita ni kuwa ulingia mtandao wa Youtube kwenye maelezo ya polisi haipo
Eneo la saba ni ushahdi wako kuwa mimi mtuhumiwa nilisema anayetaka kwenda nasi tutaenda naye na asiyetaka tutamuacha
Eneo la nane nilisema kuwa hata mimi ninayetaka kutaka kugombea urais nisahau kwenye maelezo ya polisi haipo
Eneo la tisa kwamba nilisema maneno 'no reforms no election' sijayaona kwenye maelezo yako
Eneo la kumi kwenye ushahidi wako ni maneno kuwa nilisema watasema tunafanya uasi nioneshe yako wapi kwemye maelezi yako
Tundu Lissu: 'Mheshimiwa nataka kuonesha kuwa shahidi ni muongo na hapaswi kuaminika'
Jaji - Maswali ya Dodoso
Lissu: Shahidi unanisikia?
Shahidi: Nakusikia mheshimiwa
Lissu: Naomba ujibu maswali sawa sawa na nitakavyokuuliza sawa
Shahidi: Nimeelewa
Lissu: Naomba uwaambie majaji kama uliandika maelezo polisi? Ndio au hapana
Shahidi: Ndio
Lissu: Ukioneshwa hayo maelezo yako utayatambua
Shahid: Kimya…kisha ndio ninaweza kuyatambua
Lissu: Uliyasaini?
Shahidi: Sikumbuki
Lissu: Mheshimiwa jaji naomba shahidi aoneshwe maelezo yake
Kimya kwa muda mahakamani wakati shahidi alikipelekewa maelezo yake
Lissu: Umepata maelezo yako shahidi?
Shahidi: Ndio nimepata
Lissu: Waeleze kama ndio maelezo uliyoandika polisi Songea
Shahidi: Ndio
Lissu: Waeleze kama yana sahihi yako
Shahidi: Ndio ipo Lissu: Waeleze majaji kama ni ya tarehe 25/04/2025
Shahidi: Sioni
Lissu: Angalia juu ya karatasi maneno yanayosomeka maelezo yametolewa tarehe 25 mwezi wa nne 2025
Shahidi: Sioni
Lissu: Mheshimiwa nataka kuonesha kuwa shahidi ni muongo na hapaswi kuaminika Waheshimiwa majaji ninaomba nimsomee maelezo yake sawa shahidi
Shahidi: Sawa!
Tundu Lissu anasoma maelezo yote ya shahidi
Shahidi: 'Nilikuwa nimevalia T-shirt yangu ya 'No Reform No Election'
Wakili: Pia nini kilifuata?
Shahidi: Ulifanyika utaratibu kupata tisheti hizo toka Dar es salaam hadi kutufikia Wakili: baada ya hapo nini kiliendelea?
Shahidi: Baada ya utaratibu huo tuambizana tutakutana tarehe 20 kwa matembi hayo ya hiari Wakili: Baada ya kufika tarehe 20 nini kilifuata?
Shahidi: Tulikusanyika
Wakili: Kabla ya matembezi majira ya asubuhi siku hiyo unakumbuka nini Shahidi: nakumbuka tulivaa tisheti tulizoagiza kutoka Dar
Wakili: baada ya kupata T shirt
Shahidi: Tulikubaliana matembezi itakuwa jioni kwa ajili ya matembezi
Wakili: Na hiyo taarifa uliipata wapi?
Shahidi: Kwenye group
Wakili: Sasa mlikubaliana mkutane wapi?
Shahidi: Sehemu moja songea panaitwa kwa Dis kitimoto
Wakili: Sasa baada ya kukutana jioni hiyo nini kilitokea?
Shahidi: Ghafla ilikuja gari ya polisi
Wakili: Twende taratibu wewe wakati unaenda kwa dis ulikuwa kwenye muonekano upi? Shahidi: Nilikuwa nimevaa tshirt yangu ya No reforms no election
Wakili: Baada ya kukutana kwa Dis Nini kilitokea?
Shahidi: Walikuja Polisi na kujitambulisha wanatoka kituo cha polisi songea na kutuambia tunatakiwa kituoni
Wakili: Nini kikafuata?
Shahidi: Walitukamata hadi kituo cha polisi Songea
Wakili: Mlipofika kituoni nini kiliendelea?
Shahidi: Nakumbuka tuliambiwa tunatuhumiwa kupanga maandamano bila ya kibali
Wakili: Baada ya kupewa tuhuma hizo nini kiliendelea?
Shahidi: Walituambia tutatoka kwa dhamana na tungetakuwa kurejea kituoni kwa RCO RUVUMA tarehe 25/04/2025
Wakili: 25:04/2025 nini kilitokea? Shahidi: 25/04/2025 Baada ya kuripoti kwa RCO alitaka tuelezee ilikuaje hadi kufika sehemu hiyo. Wakili: Mheshimiwa Jaji kwa shahidi huyu ni hayo
Shahidi P6 amemaliza kutoa ushahidi, hatua inayofuata ni mshtakiwa Tundu Lissu kuumuuliza shahidi P6 maswali ya dodoso
Kesi ya Lissu: 'Nilipata taarifa kwamba Mwenyekiti amekamatwa Wilaya ya Mbinga
Wakili: Sasa tuambie unakumbuka nini tarehe 6 april 2025 Shahidi nakumbuka nilipata taarifa mwenyekiti atakuwa na ziara mkoani ruvuma Wakali taratibu mwenyekiti ni nani
Shahidi: Mwenyekiti ni Tundu Lissu
Wakili: Hiyo taarifa ulipata wapi
Shahidi: Niliipata kwa ndugu Chiza
Wakili :Hiyo taarifa ilikutaka ufanye nini
Shahidi Ilinitaka tufanye maandalizi ya kumpokea mwenyekiti
Wakili: Nini kikafuata
Shahidi :Tulianza maandalizi na ikaeleza tarehe 10:4/2025 atakuepo Songea
Wakili :Walipanga aatakuepo wapi Songea
Shahidi: Walipanga atakuepo uwanja wa shule ya msingi Matawalo Songea
Wakili: Sasa Tarehe 9 mwezi wa nne 2025 wewe unakumbuka nini
Shihidi: Ninakumbuka nilipata taarifa kuwa mwenyekiti amekamatwa huko wilaya ya mbinga kwenye ziara Baada ya kupata taarifa nini kilitokea
Shahidi: Niliwasiliana na chiza na kumuaambia nimesikia mwenyekiti amekamatwa mbinga akanithibitishia akaniambia lakini ratiba ya mkutano wa tarehe 10/04/2025 iko pale pale jiandae ili tuwepo eneo la mkutano
Wakili :Tarehe kumi sasa mwezi wa nne 2025 nini kilitokea
Shahidi: Nakumbuka tulikusanyika uwanja wa shule ya msingi matabawe kuwasubiri viongozi waliongozwna na mwenyekiti weweze kuhutua mkutano
Wakili: Viongozi hao ni wa wapi Godbless Lema dokta slaaaa Na mwingine nani Nakumbuka pia alikuepo pia makamu mwenyekiti Heche
Wakili :nini kiliendelea
Shahidi :Nakumbuka ilikuja gari ya polisi na kututawanyisha na kwamba hakuna mkutano unaofanyika hapo na hakuna mtu anaruhusiwa kuwa eneo hilo
Wakili: Sasa baada ya kupewa katazo la polisi nini kilitokea
Shahidi: Tulielekea ofisi za chama kujua nini kifanyike kwa siku hiyo
Wakili: Hizo ofisi ziko wap
Shahidi: Ziko Songea
Wakili Songea wapi
Shahidi :Songea Mfaranyaki
Wakili :Baada ya kufika ofisini mfaranyaki nini kiliendelea
Shahidi: Nakumbuka niliwaona waandishi wa habari wakijiandaa kuongea na viongozi katika ofisi hizo Ni viongozi gani unakumbuka uliwakuta ofisini hapo
Shahidi: Namkumbuka kiongozi ndugu Abel Mayala ambaye wakati huo alikuwa mwenyekiti chadema kanda ya kusini
Wakili: vVongozi wengine unaowakumbuka Shahidi hapana ni huyo tu
Wakili: Baada ya hapo nini kiliendelea
Shahidi: Polisi wakukuja na kupiga mabomu na kututawanyisha
Wakili :Siku hiyo majira ya saa saba siku hiyo hiyo nini kiliendelea
Shahidi :Tuelekea uwanja wa shule ya msingi matabawe alikuja makamu mwenyekiti na kusema amepokea barua ya polisi kuwa kusifanye mkutano katika eneo hilo siku hiyo
Wakili :Akasemaje tena
Shahidi :Pia akasema tutawanyike eneo hilo viongozi watapanga siku ingine
Wakili: Umetuambia makamu mwenyekiti huyo makamo ni nani
Shahidi: huyo makamo ni mheshimiwa Heche
Wakili: Shahidi unakumbuka nini tareh 18/04/2025
Shahidi: Nakumbuka nilipokea taarifa kuwa tarehe 20/04/2025 ambapo ilikuwa siku ya pasaka kuwa kutakuwa na matembezi ya hiari ambapo kwenye matembezi hayo yataambatana na kuvaa tsheti zilizo andikwa no reforms no election ili kusisitiza msimamo wa chama
Kesi ya Tundu Lissu: Shahidi P6 aendelea na ushahidi
Shahidi wa siri wa Jamuhuri P6 anaendelea kutoa ushahidi
Wakili: Eleza mahakama ulipokuwa kwenye mtandao wa youtube ulikuwa unafanya nini Shahidi: Kwenye Youtube niliingia kwenye akaunti ya jambo TV
Wakili: Baada ya kuingia Jambo TV?
Shahidi: Nilifanikiwa kuona video ya hotuba ya mwenyekiti wa chama cha Chadema akiwa anahutubia watu kwamba bila ya mabadiliko hakuna uchaguzi hivyo 'tunaenda kukinukisha tunakwenda kuvuruga uchaguzi', pia nilisikia na kuona akisema 'tunakwenda kukinukisha na yeyote ambaye atakuwa pamoja nasi tutaenda naye ambaye hatotaka tutamuacha' pia alisema 'kama kuna mtu yeyote anatarajia kugombea udiwani asahau' pia alisema 'yeyote anayetarajia kugombea ubunge pia asahau' akaendelea kusema 'hata mimi mwenyekiti kuhusu kugombea urais hilo sahau' pia akasema 'bila ya mabadiliko hakuna uchaguzi'
Wakili: Kingine kipi alisema? pia akasema 'watasema tunafanya uasi, ni kweli ni uasi bila ya mabadiliko hakuna uchaguzi'
Wakili: Alikuwa anazungumza kwenye mazingira gani?
Shahidi: Ilikuwa ukumbini sehemu aliposimama nyuma kulikuwa na bendera ya taifa na bendera ya Chadema pembeni
Wakili: Lissu alikuwa kwenye muonekano gani siku hiyo
Shahidi: Alikuwa amevaa kombati ya kaki
Wakili: Huyo Tundu Lissu wewe unamfahamu vipi?
Shahidi: Namfahamu kama mwanasiasa mkongwe na maarufu
Wakili: Baada ya kuona na kusikia hiyo video nini kilifuata?
Shahidi: Maneno yake yaliniingia na kunishawishi kuwa miongoni mwa wale watakaounga mkono ajenda ya kuzuia uchaguzi pasipo na mabadili
Wakili: Kuzuia vipi uchaguzi
Shahidi: kuzia uchaguzi kwa maana ya kukinukisha
Wakili: Na hiyo ajenda ambayo unasema ulishawishika ni ipi?
Shahidi: Ajenda ya kukunukisha ni kwamba kufanya vurugu au kuharibu uchaguzi
Wakili: Shahidi umezungumza kuhusu uchaguzi huo uchaguzi ni upi?
Shahidi: Uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 ambao unahusisha madiwani wabunge na Rais
Wakili: Baada ya kushawishika na hotuba ya mwenyekiti wewe ulichukuwa hatua gani
Shahidi: Niliamua kumfuata mwenyekiti wa vijana ambaye ni maarufu kama mwamba wa kigoma nikamweleza nia yangu na namna nilivyoshawishika na maneno ya mwenyekiti na kutamani kuwa miongoni mwa watu tutakao kinukisha kutafuta mabadiliko kabla ya uchaguzi Wakili: Baada ya kumuambia nia yako hiyo nini kiliendelea?
Shahidi: Alinisifia na kunipongeza kwa huo ushujaa
Wakili: Nini kiliendelea
Shahidi: Alinipongeza akaniambia vijana kama ninyi ndio mnatakiwa kulikombia taifa
Wakili: Nini kilifuata
Shahidi: Aliniambia kitakachofuata kuhusu harakati hizo za kukinukisha atanishirikisha na pia aliniahidi ataniunganisha na makundi mbalimbali yanayojadili mipango ya kudai mabadiliko kabla ya uchaguzi
Wakili: Group lipi ambalo uliwekwa
Shahidi: Nakumbuka ni kundi la siasa yetu update
Wakili: Baada ya hapo nini sasa kilifuata
Shahidi: Nilendelea na shughuli zangu na yeye akaendelea na shughuli zake
Kesi ya Tundu Lissu: Yaliojiri hapo Jana kwa ufupi

Iwapo unajiunga nasi kwa mara ya kwanza, hapo jana siku ya Alhamisi kesi iliahirishwa baada ya mshitakiwa kusema hajala
Wafuasi wake waliokuwa mahakamani waliangua kilio baada ya kusikia kauli hiyo.
Awali shahidi wa kwanza alisema kwamba 'alliona video ya Lissu akisema atakinukisha na uchaguzi mkuu hautafanyika' - Shahidi
Vilevile aliongezea kwamba 'aliihofia video hiyo ingesababisha uvunjifu wa amani, kukwamisha biashara na kusababishia njaa'.
Hatahivyo akimjibu Tundu Lissu alisema Nukisha inatokana na neno nuka na kwamba inaweza kuwa harufu nzuri au harufu mbaya
Tundu Lissu ambaye anajiwakilisha katika kesi hiyo alimuuliza shahidi huyo kuhusu video aliyokuwa akiitazama Facebook ilikuwa kwenye akaunti ya nani wakati alipokua anaiperuzi….
Shahidi alimjibu akisema hakufahamu kupitia account gani
Mashahidi 5 kati ya 30 wanatoa ushahidi katika kesi ya Tundu Lissu leo ambapo anashtakiwa kwa makosa ya uhaini.
Uhaini ni kesi ambayo ukipatikana na hatia hukumu yake inaweza kuhusisha kunyongwa hadi kufa
Lissu alikamatwa April mwaka jana mkoani Iringa kwenye shughuli za chama akituhumiwa kwa kesi ya mbili za uhaini na kesi nyingine ya uchochezi.
