Majibu ya maswali magumu kuhusu hedhi

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Licha ya taarifa nyingi zinazopatikana mtandaoni leo, bado kuna maswali mengi kuhusu hedhi.

Watu wengi hawataki kuzungumza wazi juu ya mada hii.

Matatizo yanayohusiana na hili bado pia yako pale pale.

Tumejaribu kupata majibu kwa baadhi ya maswali yaliyotafutwa sana kwenye mtandao wa Google kuhusiana na hedhi.

Hata hivyo, ikiwa unajihisi vibaya wasiliana na daktari.

Usiwahi kunywa dawa bila maagizo ya daktari.

1. Ni kiwango gani cha damu hutoka wakati wa hedhi?

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Kutokwa na damu ni sehemu ya mzunguko wa hedhi wa wanawake.

Kulingana na Huduma ya Kitaifa ya Afya ya Uingereza (NSS), 30 hadi 72 ml ya damu hutoka wakati wa hedhi.

Hiyo inamaanisha ni kuanzia vijiko vitano hadi 12.</b> <i>Bleeding may be heavier in some women.

Kutokwa na damu kunaweza kuwa nzito kwa wanawake wengine.

Kawaida damu hii ni nyekundu au nyeusi au hudhurungi kwa rangi.

Pia inaonekana nyekundu wakati damu ni nyingi.

2. Je, mzunguko wa hedhi huchukua siku ngapi?

Kwa kawaida, hedhi huanza mara moja kila baada ya siku 28.

Lakini, kwa watu wengine inaweza kuchukua kati ya siku 21 hadi 40.

3. Kwa nini damu inatoka sana na nini kifanyike?

Hauhitaji Whatsapp
BBC Swahili sasa kwenye WhatsApp

Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.

Bonyeza hapa kujiunga

Mwisho wa Whatsapp

Hedhi nzito pamoja na kutokwa na damu hujulikana kama ‘menorrhagia’ au hedhi nzito.

Kunaweza kusabbaishwa na mengii.

Kutokwa na damu zaidi ya 80 ml inaitwa ‘menorrhagia’.

Hii inaweza kutambuliwa na baadhi ya vipengele.

Dalili kama vile kutokwa na damu iliyoganda, kubadili pedi kila saa, maumivu ya tumbo ambayo hayapungui hata baada ya kutumia dawa huonekana kwa waathirika.

Hii inaweza kutokea kwa sababu ya mabadiliko katika mfuko wa uzazi, kiwango cha kimetaboliki, na homoni.

Wanawake wengine hupata hedhi nzito wanapokaribia kukoma hedhi.

Kushuka kwa kiwango cha homoni na matatizo kama vile kuwepo kwa uvimbe kwenye mfuko wa uzazi kunaweza pia kusababisha tatizo hili.

Kwa upande mwingine, hedhi nzito inaweza pia kutokea wakati vigandisha damu katika damu zinapungua.

Tatizo hili linaweza pia kutokea wakati mtu anakunywa dawa za kupunguza damu.

Kutokwa na damu kunaweza kutokea mara kwa mara wakati una maambukizi fulani au kama kunywa dawa fulani.

Madaktari wanapendekeza kula mboga mboga na viazisukari ambayo ina madini mengi ya chuma ili kupunguza tatizo hili.

Pia inasemekana ni muhimu kufanya mazoezi ya dakika 30 hadi 40 kwa siku.

Madaktari pekee wanaweza kuagiza aina gani ya dawa utahitaji.

.

Chanzo cha picha, Getty Images

4. Je kuna siku ngapi kwa mwezi?

Hedhi inaweza kuwa kutoka siku 3 hadi 8.

Kawaida hudumu siku tano kwa watu wengi.

Damu huwa nzito wakati wa siku mbili za kwanza.

5. Je, hedhi huanza lini?

Kwa kawaida hedhi huanza katika umri wa miaka 12 kwa wasichana.

Hata hivyo, katika wasichana wengine inaweza kuanza mapema kidogo na kwa wengine inaweza kuchelewa.

Kufikia umri wa miaka 16 au 18, hedhi huanza kuja mara kwa mara.

Inaweza pia kucheleweshwa kwa sababu fulani.

6. Mayai yanatolewa lini?

Wakati wa kujifunza kuhusu mzunguko wa hedhi, watu wengi pia huuliza maswali yanayohusiana na ujauzito.

Wakati mimba hutokea kwa wanawake, mwezi pia unachukuliwa kuhesabu wakati ulianza.

Kawaida, mayai hubaki kwenyemfuko wa uzazi wakati wa hedhi kwa wanawake.

Mayai haya yana uwezekano wa kutolewa siku 12 hadi 14 kabla ya kipindi kinachofaa.

Kulingana na taarifa za NHS, seli za mbegu za kiume hubaki hai katika mwili wa mwanamke kwa takriban siku saba.

Ikiwaitashikana na yai kabla ya hili, mimba hutokea.

Kwa wakati huu, yaani siku 12 hadi 14 kabla ya hedhi, uwezekano wa mimba ni mkubwa.

Uwezekano wa kupata mimba mara baada ya hedhi ni mdogo, hata hivyo, haiwezi kuzingatiwa kuwa hii haitatokea.

7. Je, unaweza kufanya ngono wakati wa hedhi?

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Ngono wakati wa hedhi inachukuliwa kuwa mbaya katika jamii ya Kihindi.

Uchunguzi wa kina umefanywa juu ya hili katika nchi za magharibi.

Utafiti katika nchi za Magharibi unaonyesha kuwa hakuna ubaya katika kufanya hivi.

Asilimia 55 ya washiriki 500 katika utafiti walisema kuwa kufanya ngono wakati wa hedhi ni hisia mpya.

Hata hivyo, asilimia 45 iliyobaki walieleza kwamba hawakuhisi hisia hizo.

8. Ni chakula gani kinapaswa kuchukuliwa ili kupata hedhi?

Chakula tunachokula kinahusiana kwa karibu na mzunguko wetu wa hedhi.

Kula mlo kamili kunaweza kudhibiti mzunguko wa hedhi usio wa kawaida.

Hata hivyo, ikiwa tatizo tayari limeongezeka, wasiliana na daktari.

Vitafunio huathiri homoni zinazoathiri mzunguko wa hedhi.

Hii inaweza kusababisha kuchelewa kwa hedhi au vipindi virefu.

9. Je, ni madhara gani ya vidonge vya kuchelewesha kupata hedhi?

Wanawake mara nyingi huchukua vidonge vya kudhibiti uzazi wakati wa sherehe.

Hata hivyo, Dk Gauri Pimpalkar, Daktari Binakolojia katika Hospitali ya Sahyadri huko Nashik, anasema madaktari karibu kamwe hawaagizi tembe kama hizo.

Kuna aina mbili za homoni katika mwili wa wanawake ziitwazo estrojeni na progesterone.

Kwa msingi wa haya, hedhi huja kila mwezi.

Hata hivyo, kuchukua vidonge hivi vya homoni kunaweza kuchelewesha mzunguko wa hedhi.

Hii ina maana kwamba vidonge hivi vinaharibu mzunguko wa homoni.

"Ina madhara mengi, alisema Gowri, "Ikiwa unatumia tembe hizo mara kwa mara, kuna hatari ya kupooza".

Wanawake wengine hunywa dawa hizi kwa siku kumi hadi 15.

Ni muhimu kuzingatia historia ya afya ya wagonjwa wakati wa kuagiza tembe. Ni bora kutotumia tembe hizi ikiwa una matatizo kama vile kipandauso, shinikizo la damu na kupungua kwa uzito.