‘Siwezi kuunga mkono vita’ - Mkuu wa Kituo cha Kupambana na Ugaidi Marekani ajiuzulu
Afisa mkuu wa Marekani anayeshughulikia mapambano dhidi ya ugaidi nchini Marekani Joe Kent, ametangaza kujiuzulu nafasi hiyo akisema "Nikiwa na nia njema, siwezi kuunga mkono vita vinavyoendelea nchini Iran".
Seneti ilimthibitisha Joe Kent kama chaguo la Trump kwa nafasi hiyo Julai iliyopita.
Katika katika barua yake ya kujiuzulu kwenda kwa Trump, Kent anasema: "Iran haikuwa tishio lolote kwa taifa letu, na ni wazi kwamba tulianzisha vita hivi kutokana na shinikizo kutoka kwa Israeli na ushawishi wake wenye nguvu kwa Marekani."
"Ninaunga mkono maadili na sera za kigeni ulizofanya kampeni mwaka 2016, 2020, 2024, ambazo ulizitekeleza katika muhula wako wa kwanza."
"Hadi Juni 2025, mlielewa kwamba vita vya Mashariki ya Kati vilikuwa mtego ulionasa maisha ya thamani ya wazalendo wetu wa Marekani na kupunguza utajiri na ustawi wa taifa letu."
"Kama mkongwe aliyejitolea kupigana mara 11 na kama mume wa ‘Gold Star’ niliyempoteza mke wangu mpendwa Shannon katika vita vilivyotengenezwa na Israeli, siwezi kuunga mkono kupeleka kizazi kijacho kupigana na kufa katika vita ambavyo haviwanufaishi watu wa Marekani wala havihalalishi gharama ya maisha ya Wamarekani."