Trump awaita washirika wa Nato 'waoga'

Mlango-Bahari wa Hormuz umefungwa huku Iran ikishambulia meli za mafuta katika eneo hilo tangu vita kuanza.

Muhtasari

Moja kwa moja

Abdalla Seif Dzungu & Asha Juma

  1. Asante kwa kuwa pamoja nasi. Kwaheri kwa sasa.

  2. Chuck Norris afariki dunia akiwa na umri wa miaka 86

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Mwigizaji na msanii wa mapigano ya judo, Chuck Norris alifariki dunia jana asubuhi akiwa na umri wa miaka 86, familia yake imetangaza kupitia mtandao wa Instagram.

    Norris alilazwa hospitalini huko Hawaii kabla ya kifo chake

    Norris alilazwa hospitalini huko Hawaii kwa dharura ya kimatibabu kabla ya kifo chake, TMZ iliripoti hapo awali.

    Katika taarifa yao, familia yake ilisema wanapendelea kuweka hali hiyo kuwa ya siri, lakini walielezea kifo cha Norris kama kilichotokea "ghafla".

    'Hamkuwa mashabiki tu, mlikuwa marafiki zake' - taarifa kamili ya familia

    Tunasikitika kama familia kutangaza kifo cha ghafla cha mpendwa wetu Chuck Norris kilichotokea jana asubuhi. Ingawa tungependa kuweka hali hiyo kuwa ya faragha, tafadhali jua kwamba alikuwa amezungukwa na familia yake na alituacha akiwa na amani.

    "Kwa ulimwengu, alikuwa msanii wa mapigano ya judo, mwigizaji, na nembo ya nguvu. Kwetu, alikuwa mume aliyejitolea, baba na babu mwenye upendo, ndugu wa kipekee, na kitovu cha familia"

    Aliishi maisha yake kwa imani, kusudi, na kujitolea bila kuyumba kwa watu aliowapenda. Kupitia kazi yake, nidhamu, na wema wake, alitoa hamasa kwa mamilioni duniani kote na mchango wake utakumbukwa na wengi daima.

    Ingawa mioyo yetu imeumia, tunashukuru sana kwa maisha aliyoishi na kwa nyakati zisizosahaulika tulizobarikiwa kushirikishana naye. Upendo na uungwaji mkono aliopata kutoka kwa mashabiki kote ulimwenguni ulikuwa na maana kubwa kwake, na familia yetu inawashukuru sana kwa hilo. Kwake, hamkuwa mashabiki tu, mlikuwa marafiki zake.

    Tunajua wengi wenu mmesikia kuhusu kulazwa kwake hospitalini hivi karibuni, na tunashukuru sana kwa maombi na usaidizi mliompa.

    Tunapoomboleza msiba huu, tunaomba faragha kwa ajili ya familia yetu wakati huu. Asante kwa kumpenda pamoja nasi.

  3. Trump awaita washirika wa Nato 'waoga'

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Rais wa Marekani Donald Trump, amewaita washirika wa Nato "waoga" na kusema itakuwa "rahisi" kwao kusaidia kufungua njia ya meli katika Mlango-Bahari wa Hormuz.

    Katika akaunti yake kwenye mtandao wa Truth Social aliandika:

    "Bila Marekani, NATO NI DHAIFU! Hawakutaka kujiunga na mapigano kuizuia Iran Inayotumia Nyuklia."

    "Kwa kuwa tumeshinda mapigano kijeshi, bila kuwahatarisha pakubwa, wanalalamika kuhusu kupanda kwa bei za mafuta wanakolazimika kulipa, lakini hawataki kusaidia kufungua Mlango-Bahari wa Hormuz, mbinu rahisi ya kijeshi ambayo ndiyo sababu pekee ya kupanda kwa bei za mafuta."

    "Ni rahisi sana kwao kufanya hivyo, bila hatari kubwa. WAOGA, nasi tutakumbuka!"

    Soma zaidi:

  4. Raia wa Iran akamatwa akijaribu kuingia kambi ya nyuklia ya Uingereza

    .

    Chanzo cha picha, PA Media

    Mwanamume mmoja kutoka Iran amekamatwa na mwanamke mmoja baada ya kujaribu kuingia katika kambi ya jeshi la majini ya Faslane, makao makuu ya manowari za Uingereza zenye silaha za nyuklia.

    Polisi huko Scotland walisema mwanamume mmoja mwenye umri wa miaka 34 na mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 31 walikamatwa katika Kituo cha Wanamaji cha HM Clyde yapata saa 17:00 siku ya Alhamisi.

    Uraia wa mwanamke huyo haujulikani.

    Jeshi la Wanamaji la Kifalme lilisema washukiwa "walijaribu bila mafanikio" kuingia kwenye kambi hiyo, karibu na Helensburgh, Argyll na Bute.

    Soma zaidi:

  5. Waziri Mkuu wa Australia azomewa msikitini

    .

    Chanzo cha picha, AUSTRALIAN BROADCASTING COMPANY / REUTERS

    Waziri Mkuu wa Australia Anthony Albanese amezomewa wakati wa ziara yake katika msikiti mkubwa zaidi nchini humo kwa ajili ya sala ya Eid al-Fitr, wakielezea ghadhabu yao juu ya msimamo wake kuhusu mashambulizi ya Israeli huko Gaza.

    Baadhi ya Waislamu na Wayahudi wa Australia wamekasirika juu ya msimamo wa serikali ya mrengo wa kati kushoto tangu vita vya Gaza vianze, wakielezea wasiwasi wao kwa Wapalestina, ambaye amekuwa akihimiza kusitishwa kwa mapigano mara kwa mara, na kuunga mkono haki ya Israeli ya kujilinda.

    Video zilionyesha waandamanaji wakipaza sauti zao kwa hasira wakati ibada inaendelea yapata dakika 15 baada ya Waziri wa Mambo ya Ndani wa Albania Tony Burke kujiunga na waumini katika Msikiti wa Lakemba magharibi mwa Sydney kuadhimisha mwisho wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

    Waumini walimzomea, wakawaambia Albanese na Burke "Tokeni nje!" na kuwaita "wanaopendelea mauaji ya kimbari", wakimaanisha mauaji ya Wapalestina yanayotekelezwa na Israeli huko Gaza, kufuatia shambulizi la wanamgambo wa Hamas mnamo 2023.

    "Ndugu na kina dada wapendwa, tulieni kidogo," mmoja wa waandaaji aliambia umati, akiwahimiza watu kukaa chini na kuacha kurekodi kipindi wanarusha maneno. "Ni Eid. Ni siku ya furaha."

    Soma zaidi:

  6. Iran yaiambia Uingereza kutoa kambi zake kwa Marekani ni 'uchokozi'

    .

    Chanzo cha picha, NurPhoto via Getty Images

    Iran imeiambia Uingereza kwamba kuruhusu Marekani kutumia kambi za kijeshi za Uingereza kutachukuliwa kama "kushiriki katika uchokozi", kulingana na wizara ya mambo ya nje ya Iran.

    Iran inasema Waziri wa Mambo ya Nje Abbas Araghchi alifanya mazungumzo na mwenzake wa Uingereza Yvette Cooper, ambapo alisema kwamba msaada wowote utakaotolewa na Uingereza kwa Marekani utasababisha "kuongezeka kwa mzozo huo".

    Araghchi aliishutumu Uingereza na mataifa mengine ya Ulaya kwa "mbinu ya upendeleo" kuelekea kile anachokielezea kama "uchokozi wa wazi" kutoka kwa Marekani na Israel.

    Inaripotiwa kwamba Araghchi pia aliikosoa Uingereza kwa kushindwa kulaani mashambulizi ya Israel kwenye viwanda vya gesi vya South Pars vya Iran.

    Bado hatujasikia kutoka kwa serikali ya Uingereza kuhusu hili. BBC imeiomba ofisi ya mambo ya nje ya Uingereza kutoa maoni.

    Soma zaidi:

  7. 'Kuingia kwa nguvu uwanjani' wakati wa mechi ya soka kuwa kosa la jinai Uingereza

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Kuingia katika mechi ya soka nchini Uingereza na Wales bila tikiti itakuwa kosa la jinai chini ya sheria mpya zinazoanza kutekelezwa kabla ya fainali ya Kombe la Carabao Jumapili kati ya Arsenal na Manchester City katika Uwanja wa Wembley.

    Wahalifu watapigwa marufuku kutazama mpira wa miguu kwa hadi miaka mitano, pamoja na kupigwa faini ya hadi pauni 1,000.

    Sheria hiyo imeanzishwa kutokana na vurugu kubwa iliyoharibu fainali ya Mashindano ya Ulaya kati ya Uingereza na Italia huko Wembley mnamo Julai 2021, ambapo maelfu ya mashabiki waliingia uwanjani kwa nguvu.

    Sheria mpya imeundwa ili kudhibiti wachezaji 'kuingia kwa nguvu uwanjani' - ambapo wafuasi wasio na tiketi hupitia kwenye lango na kubaki karibu na walionunua tiketi kwa njia halali.

    Pia itakuwa kinyume cha sheria kujaribu kimakusudi kuingia kwa kutumia tiketi bandia, pasi na hati za uidhinishaji, au kwa kujifanya mfanyakazi.

    Hadi kufikia sasa, hakujakuwa na adhabu maalum za kisheria kwa kuingia kwenye mechi ya mpira wa miguu bila tikiti, huku mashabiki wanaopatikana wakifanya hivyo wakifukuzwa bila kuchukuliwa adhabu nyingine yoyote.

    Watu sitini na tisa walikamatwa kuhusiana na fainali ya Kombe la Carabao mwaka jana, huku Polisi wa Jiji wakithibitisha wakati huo kwamba idadi kubwa ya waliokamatwa walikuwa wakijaribu kuingia Wembley bila tikiti. Lakini hadi kufikia sasa, imekuwa vigumu kwa polisi kuendeleza kesi hizo.

    Soma zaidi:

  8. Wairan washerehekea mwaka mpya wa Kiajemi 'bila intaneti'

    .

    Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

    Iran inaadhimisha ‘Nowruz’, Mwaka Mpya wa Kiajemi wakiwa "bila mtandao" huku kukatika kwa intaneti nchini humo kukishuhudiwa kwa siku 21 kufikia sasa, kundi la ufuatiliaji wa intaneti la NetBlocks linaripoti.

    .

    Chanzo cha picha, NetBlocks

    NetBlocks iliripoti siku ya Alhamisi kwamba kuminywa kwa intaneti sasa kumechukua muda mrefu zaidi katika historia ya Iran, kuliko mtandao ulivyofungwa wakati wa maandamano mwezi Januari.

    Soma zaidi:

  9. Afisa wa Kikosi cha Iran auawa katika shambulizi - vyombo vya habari

    .

    Chanzo cha picha, AFP

    Msemaji na afisa wa uhusiano wa umma wa Kikosi cha Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) ameuawa katika mashambulizi ya Marekani na Israeli, vyombo vya habari vya Iran vinaripoti.

    Ali Mohammad Naini alihudumu katika kikosi cha IRGC kwa miongo minne, akihudumu kama msemaji wa shirika hilo kwa miaka miwili iliyopita, linaripoti shirika la habari la Fars linaloshirikiana na IRGC.

    Milipuko mikubwa zaidi yaripotiwa Tehran

    Israeli imekuwa ikishambulia mji mkuu wa Iran, Tehran, kwa mashambulizi ya anga huku Wairani wakisherehekea Nowruz - Mwaka Mpya wa Uajemi.

    Usiku kucha, Iran pia ilirusha makombora kuelekea Yerusalemu. Milio mikubwa ya uzuiaji ilisikika mara kwa mara juu ya ardhi usiku kucha.

    Waziri Mkuu wa Israeli, Benjamin Netanyahu hapo awali aliwaambia waandishi wa habari kwamba Iran sasa "imesambaratishwa" na haiwezi kurutubisha madini ya urani au kutengeneza makombora ya balestiki.

    Wiki hii, Iran ilipolipiza kisasi kwa shambulio la Israeli kwenye kiwanda chake kikubwa cha gesi cha South Pars, bei za mafuta duniani zilipanda. Sasa zimeanza kushuka kutokana na ahadi ya Israeli ya kujiepusha na mashambulizi kama hayo na mipango ya Marekani ya kuongeza uzalishaji wa mafuta.

    Pia kulikuwa na taarifa ya pamoja Alhamisi jioni, ambapo Uingereza, Ufaransa, Japani na wengine walielezea kile walichosema ni "utayari wao wa kuchangia juhudi stahiki ili kuhakikisha usalama" katika Mlango-Bahari wa Hormuz.

    Soma zaidi:

  10. Qatar yakashifu shambulio la Iran kwenye mfumo wake wa gesi

    Wizara ya Mambo ya Nje ya Qatar imelaani shambulio la Iran lililolenga Ras Laffan kituo kikubwa cha kuuza gesi asilia iliyoyeyushwa (LNG) na kutaja hatua hiyo “kuongezeka kwa hatari” na “kiburi kisichokubalika” kinachohatarisha utulivu wa kanda hiyo.

    Wizara ya Mambo ya Nje ya Qatar ilisema katika chapisho kwenye mitandao ya kijamii kuwa mashambulizi ya Iran dhidi ya Qatar yanachochea mgogoro zaidi eneo hilo.

    Sheikh Mohammed bin Abdulrahman Al Thani, ambaye ni waziri mkuu na pia waziri wa mambo ya nje, alisema: “Vitendo vya kigaidi kama hivi, vya kupanua vita hivyo vitaongeza mgogoro katika kanda hii.”

    Aliongeza kuwa usalama wa kanda ni “wajibu wa kila mmoja”.

    Baada ya Israel kushambulia eneo la gesi asilia la South Pars nchini Iran siku ya Jumatano,

    Tehran ililipiza kisasi kwa kushambulia vituo vya nishati nchini Qatar.

  11. Israel yaanzisha wimbi jipya la mashambulizi dhidi ya Iran licha ya kukatazwa kufanya hivyo na Marekani

    .
    Maelezo ya picha, Netanyahu

    Israel imezindua wimbi jipya la mashambulizi dhidi ya Iran mapema leo, siku moja tu baada ya Rais Donald Trump kuwaonya wasirejelee mashambulizi yao dhidi ya miundombinu ya gesi asilia ya Iran.

    “Nilimwambia, usifanye hivyo, na hatafanya hivyo,” Donald Trump aliwaambia waandishi wa habari katika ofisi yake hapo jana.

    Baadaye Netanyahu alijibu kuwa Israel ilitekeleza shambulizi hilo “pekee yake” kwa kulenga uwanja wa gesi asilia wa South Pars nchini Iran, na kukubali semi za Trump kuwa alimuomba asifanye mashambulizi kama hayo tena.

    Kufuatia mashambulizi hayo ya Israel, msemaji wa jeshi la Israel IDF amesema kuwa “IDF imeanza wimbi jipya la mashambulizi dhidi ya utawala wa kigaidi mjini Tehran”

    Vita hivyo vilianza tarehe 28 mwezi Februari baada ya mazungumzo kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran kukosa kuafikia makubaliano.

  12. Milipuko na mashambulizi ya anga yaripotiwa mjini Tehran, Iran

    Israel imekuwa ikitekeleza mashambulizi ya anga kwenye mji mkuu wa Iran, Tehran, huku Wairani wakiadhimisha Nowruz mwaka mpya wa Uajemi (Persian New Year).

    Usiku kucha, Iran pia ilirusha mfululizo wa makombora kwa kulenga mji wa Jerusalem.

    Milipuko ya kudunguliwa kwa makombora hayo ilisikika usiku kucha. Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, awali aliwaambia waandishi wa habari kuwa Iran sasa haina nguvu tena ya kuzalisha makombora na madini zaidi ya Urani.

    Iran ilipojibu mashambulizi ya Israel yaliyolenga uwanja wake mkubwa wa gesi wa South Pars, bei za nishati duniani zilipanda kwa kiwango ila sasa zimeanza kushuka tena baada ya ahadi ya Israel ya kutolenga mifumo ya nishati ya Iran.

    Aidha washirika wa Marekani, Uingereza, Ufaransa na Japan, usiku wa kuamkia leo, walitoa tamko la pamoja la “Utayari wa kuchangia katika jitihada za kutoa ulinzi kwa meli zinazopita katika mlango wa bahari wa Hormuz”

  13. Marekani inafikiria kuoiondolea Iran vikwazo vya mafuta

    Huenda Marekani ikapunguza vikwazo vilivyowekwa kuhusu mafuta ya Iran, ili kudhibiti bei ya mafuta kwenye masoko ya kimataifa.

    Waziri wa Fedha wa Marekani Scott Bessent, alitoa wazo hilo katika mahojiano kwenye televisheni ya Fox, akisema hilo litahakikisha kiua mafuta ya kutosha kwa wananunuzi wa kimataifa.

    Kote duniani, bei ya mafuta imepanda kwa kiasi fulani, baada ya vita dhidi ya Iran kuanza.

    Ikiwa hilo litatekelezwa haya yatakuwa mabadiliko makubwa katika sera ya Marekani, ingawa matokeo yake hayatabiriki na huenda yasibadilishe bei ya sasa ya mafuta.

    Kabla ya vita hivyo, China ndiye alikuwa mnunuzi mkubwa wa mafuta ya Iran.

  14. Kiwanda cha mafuta cha Kuwait chashambuliwa

    Licha ya wito kutolewa kwa Iran kutolenga vituo vya nishati vya mataifa ya Ghuba, kampuni ya mafuta ya kitaifa ya Kuwait, KPC, imesema kuwa kiwanda chake cha mafuta kimeshambuliwa na ndege kadhaa zisizo na rubani.

    Kufikia sasa idadi ya vifo au majeruhi haijatangazwa. Vikosi vya dharura vinapambana kuzima moto katika kiwanda cha Mina Al-Ahmadi, huku shughuli za kiwanda hicho zikisitishwa.

    Baada ya Israel kulenga kituo cha gesi cha South Pars cha Iran, Iran imekuwa ikijibu shambulio hilo kwa kulenga mataifa ya Ghuba.

    Mashambulio haya yanaendelea wakati mataifa ya Ghuba yanaadhimisha sherehe za Eid ul-Fitr na kumalizika kwa mwezi mtukufu wa Ramadhan.

  15. Waislamu duniani kuadhimisha siku kuu ya Eid ul Fitr

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Eid ul Fitr

    Baadhi ya Waislamu wa Afrika Mashariki wanaadhimisha Eid-ul-Fitr leo Ijumaa baada ya kuelezwa kuonekana kwa mwezi Alhamisi jioni, kuashiria kumalizika kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani.

    Kaimu Kadhi Mkuu wa Kenya Sukyan Hassan alisema mwezi huo umeonekana katika maeneo kadhaa ya nchi, na uthibitisho wa kutosha kutoka Kaunti ya Kwale.

    Tangazo hilo lilitolewa na Ofisi ya Kadhi Mkuu, kuthibitisha mwanzo wa mwezi wa Shawwal na kufikisha mwisho wa siku 29 za mfungo unaozingatiwa na waumini kote nchini.

    Bwana Sukyan Hassan amesema mwezi huo umeonekana katika maeneo kadhaa ya nchi, na uthibitisho wa kutosha kutoka Kaunti ya Kwale.

    "Mwezi mpevu unaoashiria mwanzo wa mwezi wa Shawwal umeonekana kwa mafanikio jioni hii katika maeneo mbalimbali nchini. Hasa, katika Kaunti ya Kwale, haswa eneo la Ramisi, watu watatu wamethibitisha kuwa wameuona kwa wakati ufaao.

    Uaminifu wa watatu hao ulithibitishwa na imamu wa eneo hilo," Sukyan alisema.

    Ameongeza kuwa muandamo huo unakidhi matakwa ya Kiislamu yanayotumika kubainisha mwisho wa Ramadhani.

    "Mwezi wa Ramadhani umefika mwisho, na kesho itakuwa siku ya kwanza ya Shawwal na siku ya Eid-ul-Fitr," alisema.

    Nchini Tanzania, Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania Dr. Sheikh Abubakar Zubeir bin Ally Mbwana alitangaza kwamba Eid itakuwa Jumamosi baada ya mwezi kutoonekana jana Alhamis.

    Eid-ul-Fitr ni moja ya sherehe muhimu zaidi katika kalenda ya Kiislamu, kuashiria hitimisho la Ramadhani, mwezi mtukufu ambao Waislamu hufunga kuanzia alfajiri hadi jioni, hushiriki katika sala, na kutekeleza vitendo vya hisani.

  16. Milipuko yasikika Jerusalem huku Netanyahu akisema Israel 'ilichukua uamuzi peke yake' katika mashambulizi dhidi ya kiwanda cha gesi cha Iran

    .
    Maelezo ya picha, Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu

    Katika mkutano wake na wanahabari, Netanyahu alikanusha madai kuhusu uhusiano kati ya Marekani na Israel, ambao anajua unamsababishia Trump matatizo mengi. Yaani kwamba Israel iliiingiza Marekani kwenye vita na kwamba washirika hao wawili hawajafungamana kwenye malengo.

    Netanyahu alisema huu ni upuuzi kwani Trump mwenyewe alionya kwa miongo kadhaa kuhusu hatari iliyopo aliyosema Iran iliweka.

    Alipuuza maswali kuhusu chapisho la mtandao wa kijamii la Trump jana usiku, ambalo lilisema Israel haikumwambia kabla ya kulipua uwanja wa gesi wa Iran wa Pars Kusini .Maafisa wa Israel wamekiri kutekeleza shambulio hilo.

    Kuna majaribu na haya yote kuonyesha tofauti, na mvutano kati ya viongozi. Ili kuwa wazi, haya ni muhimu kwa sababu yanaweza kuwa muhimu wakati Trump anataka kujiondoa, uwezekano wa kupinga pingamizi la Israel.

    Lakini pia wanaweza kuchezewa kupita kiasi kwa sababu mtazamo wao wakati mwingine hukosa ukweli wa kimsingi zaidi kuhusu uhusiano wa Marekani na Israel - ambao unahusisha muungano uliojikita zaidi wa kijeshi unaosimamiwa na sheria za Marekani na Congress.

    Hii imeshuhudia Marekani ikiipa silaha nyingi zaidi Israeli kuliko nchi nyingine yoyote ambayo ina silaha tangu Vita vya Pili vya Dunia, na kuifanya Israeli kutawala kijeshi katika eneo hilo.

    Kila rais wa Marekani aliyetangulia amekosana kwa wakati fulani akiwa na kiongozi wa Israel.

    Picha kubwa hapa ni kwamba Trump aliamua kuwa wa kwanza kuungana na kuanzisha vita na Iran.

    Na ni wazi Trump bado anamruhusu Netanyahu udhibiti mkubwa wa jinsi Israeli inavyojiendesha.

  17. Natumai hujambo na karibu katika matangazo yetu ya moja kwa moja hii leo ikiwa siku kuu ya Eid ul Fitr nchini Kenya

Trending Now