VAR inaharibu utamu wa soka?

S

Chanzo cha picha, Getty Images

    • Author, Andy Cryer
    • Nafasi, BBC Sport Senior Journalist
  • Muda wa kusoma: Dakika 3

Mashabiki, makocha na wachezaji wa Ligi Kuu England walikumbushwa jinsi maisha yalivyokuwa huko nyuma bila kuwa na Video Assistant Referee (VAR), teknolojia ya video inayosaidia uamuzi wa uwanjani. Walikumbushwa kupitia maamuzi katika mechi za raundi ya nne ya kombe la FA.

Kwa msimu huu na ule uliopita wa Kombe la FA, VAR haikuwa inatumika hadi raundi ya tano, jambo lililowafanya mashabiki wengi kufurahia kurejea kwa soka lisilo na kusitishwa na teknolojia hiyo.

Baada ya msimu uliojaa utata, maamuzi yaliyochelewa na mkanganyiko uliosababishwa na VAR, baadhi wameanza kuhoji kama kweli mfumo huo unahitajika. Wapo wanaodai kuwa mchezo ungekuwa bora na soka lingekuwa tamu bila VAR.

Baada ya siku iliyojaa ucheleweshaji wa maamuzi, taarifa zinazochanganya na makocha wenye hasira mapema Februari, kiungo wa zamani wa Tottenham, Danny Murphy, alisema katika kipindi cha BBC Match of the Day:

"Kwa manufaa ya mchezo, ningependelea VAR iondolewe.

"Tatizo ni kile inachokifanya kwenye michezo na burudani yenyewe, hasa muda mrefu unaochukuliwa kufikia maamuzi.

Baada ya mabao kadhaa ya kuotea kuruhusiwa, penati ya wazi kukataliwa na maamuzi mengine yenye utata, mjadala kuhusu VAR umerudi tena kwenye hadhira ya wapenda soka

"Burudani tamu au maamuzi sahihi zaidi"?

C

Chanzo cha picha, Getty Images

Ushindi wenye utata wa Newcastle wa mabao 3-1 dhidi ya Aston Villa uliwapa hoja wanaounga mkono VAR na kuwa pigo kwa wale wanaoipinga.

Hauhitaji Whatsapp
BBC Swahili sasa kwenye WhatsApp

Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.

Bonyeza hapa kujiunga

Mwisho wa Whatsapp

Bao la kwanza la Tammy Abraham lilikuwa bao la wazi la kuotea, Lucas Digne wa Villa aliepuka penati ya wazi kwa mpira uliomgonga mkono, na pia angeweza kutolewa nje kwa kadi nyekundu kutokana na faulo mbaya.

Kocha wa Newcastle, Eddie Howe, alisema: "Nimechanganyikiwa kwa sababu mchezo huwa bora bila VAR kwa upande wa msisimko na burudani kwa mashabiki na sisi pia.

"Lakini VAR hutoa matokeo sahihi zaidi. Inaifanya michezo kuwa ya haki zaidi katika maamuzi."

Kocha wa Aston Villa, Unai Emery, alisema wazi: "VAR ni muhimu. Inahitajika kuwasaidia waamuzi."

Katika mechi ya Liverpool dhidi ya Brighton pia kulikuwa na maamuzi ya utata. Bao la Rio Ngumoha lilikataliwa kimakosa kwa kuotea, huku Brighton wakikasirishwa na penati aliyopewa Mohamed Salah.

Kocha wa Liverpool, Arne Slot, alisema: "Kwa ujumla, napenda kutazama soka bila VAR kwa sababu ukifunga unajua ni bao moja kwa moja.

"Ningependa VAR itumike tu kwa mambo yaliyo wazi kabisa kama kuotea au mpira kuvuka mstari wa goli. Mengine waachiwe waamuzi."

Pep Guardiola wa Manchester City alisema hana uhakika kama soka ni tamu au bora likiwa na VAR au bila VAR:

"Wakati mwingine naona ni bora, wakati mwingine nahisi VAR inasaidia kufanya mchezo uwe wa haki zaidi. Kwa kweli sijui."

Waamuzi wenalemazwa na VAR sasa?

C

Chanzo cha picha, Getty Images

Wengine wanaamini tatizo si VAR, bali ni waamuzi kutotekeleza majukumu yao ipasavyo.

Alan Shearer alisema:

"Ningependa waamuzi wafanye kazi yao vizuri. Si jambo kubwa sana kuomba hilo.

"Kama unataka ushahidi wa madhara ya VAR kwa waamuzi, Jumamosi ni mfano mzuri. Wanaonekana kuogopa kufanya maamuzi bila kuwa na 'kinga' ya VAR."

Lakini Shay Given alisema: "Hii inaonyesha kwa nini tunahitaji VAR. Maamuzi mengi yalikuwa mabaya. VAR ni msaada hata kama tunailalamikia mara nyingi."

Kocha Howe alikubali kuwa kuna uwezekano wa waamuzi kutegemea VAR kupita kiasi:

"Kuna hoja ya kusema ndio. Wakati VAR ipo, unaweza kufikiria 'sitatoa maamuzi sasa, VAR itaangalia'. Hilo linaweza kupunguza umakini wa maamuzi."

Hata hivyo, mwamuzi wa zamani Graham Scott alikataa wazo kuwa waamuzi wanajificha nyuma ya VAR:

"Sidhani kama hilo ni la haki. Michakato yao haibadiliki sana.