Israel yasitisha mashambulizi katika eneo la utafutaji marubani nchini Iran - ripoti
Jeshi la Israel limeahirisha mashambulizi katika eneo la Iran ambapo utafutaji wa marubani wa ndege za kivita za Marekani unaendelea, kulingana na ripoti kutoka CNN, shirika la habari la AP na Channel 12 ya Israeli.
CNN inasema afisa wa Israeli alisema kwamba mashambulizi yameahirishwa katika eneo la utafutaji, huku Channel 12, ikimnukuu afisa mkuu wa Israel, ikiripoti kwamba mashambulizi yote yamesitishwa. AP pia iliripoti kwamba mashambulizi ya angani yamesitishwa katika maeneo husika kutokana na juhudi za uokoaji.
AP inasema afisa huyo wa Israeli alizungumza nao kwa sharti la kutotajwa jina "kwa sababu operesheni hiyo inaendelea".
Jeshi la Ulinzi la Israeli halijathibitisha ripoti hizi.
Soma zaidi: