Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Thailand:Kombe la EFL kuitwa Carabao Cup
Michunao ya kombe la ELF cup ya nchini England kwa sasa itajulika kama Carabao Cup kutokana na kupata udhamini mpya wa kampuni ya Carabao ya nchini Thailand
Kampuni hiyo inayotengeneza Kinywaji cha kuongeza nguvu mwilini imesaini mkataba wa miaka mitatu wa kudhamini michuno hiyo.
Ratiba ya kupanga droo ya mechi za raundi ya kwanza ya zamichuano hiyo itafanyika ijumaa hii huko Bangkok, Thailand.
Michezo ya kwanza itafanyika kati ya Agosti 8 na 9 nc mchezo wa fainali utapigwa katika dimba la Wembley Februari 25, 2018.
Klabu ya Manchester United ndio bingwa mtetezi wa michuano hiyo